Tuesday 20 October 2015

HAKUNA CHA KUSHEREHEKEA SIKU YA MASHUJAA

Mimi ni Mkenya mzalendo, mpenda amani. Lakini leo niruhusu nifungue roho yangu, ninene kwa ufupi.

Tunasherehekea siku ya Mashujaa, tarehe ishirini ya mwezi wa kumi kila mwaka nchini Kenya. Swali ninalouliza ni je, kuna lolote la kusherehekea?

Kama hekaya za abunuwasi zingekuwa matendo, basi taifa hili lingekuwa miongoni ma mataifa bora ulimwenguni.

Ni taifa ambalo wananchi walio kwenye mitandao ya kijamii kama vile Twitter, almaarufu Kenyans on Twitter (KOT) wana busara kuliko maafisa wa serikali.

Taifa lililojaa ubinafsi, wizi, uporaji wa mali ya umma na uroho.

Mwandishi mmoja akasema ni taifa la matajiri kumi na maskini milioni kumi. Yaani kwa kila mlalahai mmoja tuna walalahoi milioni moja.

Hamna umuhimu katika kuisherehekea siku hii, ambayo pia imebinafsishwa kwa minajili ya wachache wanaothamini tumbo zao kuliko mishahara ya wanaotoa huduma kwa wale wakenya maskini kama vile walimu.

Kama vile vyama vya kisiasa vilivyo na wafuasi, vivyo hivyo ndivyo ilivyo na maafisa wakuu katika serikali na wanaowafuata ni ndugu, jamaa na marafiki, tena sio wote, wale wa karibu.

Nchi ambayo imewatafuna, kuwala na kuwameza mashujaa wao. Kila aliyepigania haki hayupo tena, kwa kuwa watu fulani hawakuwaruhusu kuishi kuona matunda ya waliyokuwa wakipigania.

Ukweli mchungu ni kwamba, hata wangefufuka waliokufa katika kupigania uhuru - ambao hadi sasa hatujauona - bila shaka wangeanguka na kufa mara tena kutokana na mshtuko wa moyo.

Serikali za hapo awali ziliwatesa na kuwaua watu waliotaka kulikomboa taifa hili.

Yeyote aliyekataa kumbeba jogoo wake mkobani na kuwika kila asubuhi, basi alikuwa mashakani na kila aliyetaka kuwa salama, basi angeimba wimbo sawa na wa mwenye jogoo.

Jogoo angeishi miaka mia moja. Ameishi miaka hamsini na miwili sasa, safari bado ndefu kwa kuwa wenye kujua hesabu wataona wazi kuwa ana miaka mingine arubaini na nane.

Sitazungumza sana kuhusiana na historia ya mashujaa na matatizo wanayoyapitia wakenya kwa sasa, kwa kuwa sote twayafahamu vyema mambo haya.

Usifadi ndio wimbo katika kinywa cha kila Mkenya.

Mali ya Umma inachukuliwa na mababe wa uongozi. Ardhi nayo sitasema inanyakuliwa. Vijana nchini hawana kazi, hilo sitataja. Umaskini umekithiri, sisemi. Usalama haupo, hujui hilo pia?

Ufujaji wa pesa za umma ndiyo shughuli ya magavana. Pazia, Kitandazi, Lango, Rukwama, kuwahamisha watoto wanaorandaranda mitaani hadi kwenye 'Kaunti zao', nitaje tu machache.

Kazi waliyofanya mashujaa; waliouawa kikatili, yote ni bure kwa kuwa uhuru bado hatujaupata. Ukoloni mambo leo umekithiri. Walio na mali wanaongezewa. Wasio na mali hata kile kidogo walicho nacho wamenyang'anywa.

Yote tisa, kumi? Lililo na mwanzo halikosi mwisho. Nina imani na matarajio kuwa maovu haya yatakoma siku moja.

Caleb Kisabuli

Monday 12 October 2015

Meet One on One with BMW, The Able SOMU Organzing Secretary 2015/2016

Students politics has of late been associated with Money, Tribal lines and arrogance.

Well, if you thought there are no leaders out of politics but only politicians, then to some extent you were wrong because my One on One With Buya Mukonzo Winfred a.k.a BMW proved otherwise.

In her voice, I sense clear exposure of humility, transparency, accountability and electorate-oriented leadership.

Well, join me as we unleash the Capable SOMU Organizing Secretary 2015/2016.

As I sought her audience, I started by asking her who she is.

Buya is a third year student pursuing a bachelor's degree in public health. She is a brand ambassador with 'Akili Dada' initiative; a girl child empowerement organization and she is also the founding director of 'Saidia students' initiative.

Buya denies her blood and interest in politics being genetic but admits leadership is.

"The docket of the Organizing Secretary is kind of neglected and termed as irrelevant because of the roles, but it's the exact same docket that I find crucial", said BMW.

She goes ahead to say that once sworn in as the Organizing Secretary, she will ensure transparency and accountability by documenting all the SOMU activities and the documents availed to comrades at regular intervals online.

"You know how important documents are", she pauses as she takes a sip of her glass of juice which is almost halfway. "No documents, no records equals to no accountability, no transparency, and that's where corruption begins. I want to make that straight", she adds.

Asked why she chose politics, Buya wears a wide smile on her face and says "It's the only vehicle to leadership, if there were an alternative route, I would definately use it, but I'm glad I have learnt so much through politics".

She says that her desire to see change and be part of the change is what motivates her most. (Not selfish, right?) "I Always endeavor to fix that thing that I see crooked", she states.

Politics after Maseno? Yes, being an organizing secretary is only the beginning of good things to come.

Her number one role model is her dad whom she says is a great performer. "I want to follow his footsteps", she says.


#MASENODECIDES2015